Kinshasa : Watu wote wana lazimishwa ku ingiya katika maji barabarani pasipo utashi wao

Visima vya maji ya nvuwa barabarani vina patikana huku na kule mujini Kinshasa. Hali iyo ina husu raiya wenye ku ishi kandokando ya barabara toka Kinshasa handi Matadi iitwayo mu kifaransa Route de Matadi.
Visima ivyo vina sababishwa na maji ya nvuwa na vina sababisha musongano wa gari barabarani naku haribu mwenendo bora wa usafirishaji mujini Kinshasa.
Basi ku tambuka maji iyo ni hatari kubwa kwa madereva. Na wakati raiya wana tamani ku tambuka maji iyo wana bebwa mugongoni mwa vijana wamoja wenye ku omba franka za Kongo miya moja kwa kazi iyo. Vijana hao wenye ku fanya kazi yaku beba mugongoni raiya wenye ku tamani ku tambuka visima vya maji ya nvuwa hawa jali na usafi wao ingawaje franka wanao pokeya ina weza ku ishiya kwa matunzo kwani maji iyo ni chafu sana.
Madereva wa taxi wana fanya yote yawezekanao kwaajili yaku epuka visima ivyo vya maji ya mvuwa. Na hali iyo ina zorotesha mwenendo wa usafirishaji wa raiya mujini Kinshasa. Na waka madereva wamoja wana subutu ku tambuka maji iyo wana kwama naku acha gari zao katika maji iyo.
Viongongozi, kwa ngambo yao, wana gari kubwa za aina ya 4×4 waliyo nunuwa na franka ya serkali na wana ngojeya visima izo ziwe kubwa sasa mbele yaku anza kazi zaku tengeneza.












Laissez votre message !