Kinshasa : Mwenye ku shika silaa ndiye mwenye kuwa na sheria

Ina pita sasa mwezi moja jemadari moja wa FARDC ( mu kifaransa: forces armées de la République démocratique du Congo) ali hama kandokando ya makao yangu. Na nili harifiwa kuhusu ujiyo wa jirani wangu mupya katika aina yakipekee.
Siku moja kisha ku fikishwa makaoni mwangu na taxi, dereva wa taxi iyo ali pigwa na waaskari wawili wanao husika na ulinzi wa jemadari huo. Dereva uyo ali pigwa kwaani ali simamisha gari yake pembeni ya lupango ya jemadari uyo wa jeshi la Kongo. Na nili kuwa niki shuka nyumbani mwangu wakati nili sikiya fudjo mugongoni mwangu.
Nilipo rudi nyuma kwaajili yaku tambuwa ni nini… moja wa waaskari hao aka ni lalamikiya naku sema mu lingala : « Yo oyebi te que mokonzi avandaka awa, olingi kosala attentat? Soki omeki lisusu kotelemisa mutuka awa to ko tia yo na cachot… » niku sema : « Hau fahamu kama hii ni makao ya kiongozi moja ?Una tamani kutiya hapo gombora hao…? Uki subutu tena ku simamisha gari hapa tutaku weka nguvuni. »
Nilipo angaliya kandokando mwangu nika tambuwa kama hakuna chapa ao alama inayo harifu kama ina katazwa ku simamisha gari mahali pale. Lakini siku subutu sema kitu kwani nina fahamu vema namna aina ya mazungumuzo iyo ina ishaka wakati una pingana na watu hao wenye ku shika silaa.
Basi kuna ulizo moja yenye kuni gonga kichani mwangu: Yafaa ku hamisha nafasi yaku simama kwamagari kila mara kiongozi fulani ana hama katika kata fulani? Ingawaje siya safari hadi inchi zigeni ; nina jiuliza kama mambo kama hii ina endeshwa katika inchi zengine. Hapa mujini Kinshasa makao za viongozi vya jeshi ni nafasi zisiyo ruhusiwa ku wasili. Kuna hata wakati barabara nzima ina fungwa kwaani kuna kiongozi moja mwenye ku kaa hapo. Na tena ina obwa kwa raiya ku achiya njiya gari za viongozi hao wakati wana safiri barabarani hao wakati mabibi zao hao watoto wao wana pita barabarani.












Mwenye silaha, sultani ya barabara !
Laissez votre message !